Mambo ya kuzingatia wakati unapika urojo

Na Fatuma Hussein
23 Jul 2024
Urojo ni mchanganyiko wa vyakula mbalimbali pamoja na uji uji wake katika bakuli moja. Asili ya urojo ni kutoka nchini India lakini umejipatia umaurufu Tanzania pia. Leo nakupa maujanja ya kupika chakula hiki ambacho unaweza kutumia nyumbani na biashara.   Urojo wako ukiiva unaweza kuula na viazi mviringo vya kuchemsha, mayai ya kuchemsha, bagia, chachandu ya […]
article
  • Hakikisha hauachi jikoni kwa muda mrefu mpaka ukaungua.
  • Usiweke maji mengi ukawa mwepesi kupitiliza.

Urojo ni mchanganyiko wa vyakula mbalimbali pamoja na uji uji wake katika bakuli moja.

Asili ya urojo ni kutoka nchini India lakini umejipatia umaurufu Tanzania pia. Leo nakupa maujanja ya kupika chakula hiki ambacho unaweza kutumia nyumbani na biashara.  

Urojo wako ukiiva unaweza kuula na viazi mviringo vya kuchemsha, mayai ya kuchemsha, bagia, chachandu ya nazi, chipsi za muhogo, mishikaki, kachori, katlesi na pilipili. 

Tuingie jikoni

Hatua ya kwanza weka unga kwenye bakuli kisha weka maji nusu lita pamoja na binzari. Baada  ya hapo koroga hadi uhakikishe mabonge yote yameisha kisha mimina maji yaliyo baki kwenye sufuria na weka chumvi kiasi  na uache yachemke  kwa dakika 20. 

Hatua inayofuata ni kumimina uji wenye binzari kwenye maji ya moto taratibu huku ukikoroga mpaka uchanganyike. Acha uchemke kidogo kwa dakika 5 kisha mimina ndimu yako na ukoroge kidogo na hapo unaweza onja chumvi na ndimu kama zipo sawa  ndio utoe jikoni.

Kata viazi mviringo ulivyovichemsha vipande vidogo vidogo. Menya mayai kata vipande vinne, chukua bakuli na kijiko weka vipande vya viazi ulivyovikata.

Baada ya hapo malizia kuweka kachori, bagia, mishkaki, chipsi za muhogo na katlesi, kisha mimina urojo kiasi upendacho, weka chachandu ya nazi na pilipili.

Kufikia hapo urojo utakuwa tayari kwa ajili ya kutumiwa mezani. 

Unataka tukufundishe pishi gani katika makala inayofuata? Dondosha maoni yako kupitia WhatsApp namba 0750 0881 888. 

Angalizo:

  • Kama urojo ukiwa na chumvi nyingi ongeza maji. 
  • Hakikisha hauachi jikoni kwa muda mrefu mpaka ukaungua.
  • Usiweke maji mengi ukawa mwepesi kupitiliza.
© Copyright 2021 JikoPoint by Nukta Africa